Home » » UNAFAHAMU HUKUMU ALIYOPEWA JUSTIN BIEBER? TAARIFA KAMILI IKO HAPA

UNAFAHAMU HUKUMU ALIYOPEWA JUSTIN BIEBER? TAARIFA KAMILI IKO HAPA



bieber s
Hatimaye Justin Bieber amevuna matunda ya kosa alilofanya la kurusha mayai 20 kwenye nyumba ya jirani yake bila kuwa na sababu za msingi.

July 9, Justin Bieber akiwakilishwa na wakili wake aliyefahamika kwa jina la Shawn Holley amehukumiwa kufanya kazi za jamii kwa muda wa siku tano ikiwa ni pamoja na kusafisha mazingira. Pia anatakiwa kumlipa jirani yake $80,900 kama fidia ya uharibifu wa nyumba yake.

Mahakama imemtaka Justin Bieber kukaa umbali usiopungua hatua 100 na jirani yake wala familia ya jirani huyo kwa kipindi cha miaka miwili na pia ahudhurie program maalum itakayomsaidia kudhibiti hasira (enger management program).

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA NASI | 0783 561 514

 
Idrisa Bandali Available On : Facebook | Instagram | Twitter
Copyright © 2013. BANDALI 44 -Haki Zote Zimehifadhiwa
Blog Hii Imetengenezwa Na Ernest James Siwigo Inamilikiwa Na Idrisa Bandali
2brothers Inc 0719766915 | 0764214303