Home » » UNAFAHAMU HATUA ILIYOFIKIWA KUHUSU MTWARA MEDIA SACCOS ? TAARIFA IKO HAPA

UNAFAHAMU HATUA ILIYOFIKIWA KUHUSU MTWARA MEDIA SACCOS ? TAARIFA IKO HAPA

mtpc
KLABU ya waandishi wa habari mkoani hapa imekamilisha hatua muhimu katika kuanzisha chama cha kuweka na kukopa kwa wanahabari na wadau wao kitakachojulikana kama Mtwara media saccos.
Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo mipango na uchumi wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Mtwara MTPC. Godwin Msalichuma aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa hatua iliyofikiwa sasa ni ya uandikishaji wa wanachama baada ya kumaliza kuipitia rasmu ya katiba ya chama hicho.
Msalichuma alisema kuwa rasimu ya katiba iliyoandaliwa na kamati maalumu iliyoundwa kuitunga na kisha kupitiwa na waandishi na wadau wote na kuweka mapendekezo yao na hatimaye kamati ilikaa tena na kuiboresha na sasa imekamilika tayari kwa kutumika kama katiba rasmi ya chama hicho.
“Hatua ya kwanza ilikuwa kuandika katika ambayo iliandikwa na ilizinduliwa na mkuu wa wilaya ya Mtwara Wilman Ndile katika mkutano wa wadau uliofanyika januari mwaka huu…baada ya hapo ilipitiwa na wanahabari na wadau wao kisha ilirejeshwa kwa kamati ambayo imeipitia na sasa ipo tayari kwa kutmika”, alisema Msalichuma ambaye pia ni katibu msaidizi wa klabu hiyo.
Mwenyekiti huyo alisema wanahabari na wadau kadhaa wamejitokeza kujiandikisha na kujiunga na chama hicho chenye lengo la kuwajengea uwezo kiuchumi wanahabari mkoani humo ambao wengi wao ni wale ambao hawana sifa za kupata mikopo kutoka taasisi za fedha kama vile mabenki na taasisi nyingine.
“Kama mnavyofahamu wanahabari wenzangu lengo la kuanzishwa kwa chama hiki ni kuhakikisha wanahabari wanapata mikopo itakayowawezesha kuanzisha miradi ya kiuchumi na kununua vifaa vya kufanyiakazi pamoja na kujiendeleza kielimu na kusomesha watoto wao…ili litafanikiwa kama tutajiunga kwa wingi”, alisema Msalichuma.
Msalichuma alisema kuwa chama hicho kitakapokamilika kitakuwa ndio mkombozi wa kiuchumi kwa wanahabari mkoani humo ambapo kitatoa mikopo kwa masharti nafuu kwa wanachama wake ili kuwawezesha wote kukopa na mikopo hiyo itakuwa ni kwaajili ya kujiendeleza kielimu, kuanzisha miradi ya kiuchumi na kununua vifaa vya kufanyiakazi.
Akizungumzia masharti ya kujiunga mwenyekiti huyo alisema kuwa wanaoruhusiwa kujiunga ni wanahabari wote wanaoishi na kufanyakazi zao ndani ya mkoa wa Mtwara bila kujali ni wanachama wa MTPC au hapana, wafanyakazi wote wanaofanyakazi katika vituo vya redi ambao sio waandishi wa habari pamoja na wadau wa habari wanaoishi mkoani humu.
Aidha Msalichuma alisema kuwa chama hicho ambacho kwa sasa kinaendeshwa chini ya uongozi wa juu wa MTPC kinatarajiwa kupata viongozi wake miezi mitatu ijayo ambapo kitafanya mkutano mkuu wa kwanza wa uchaguzi na kuwapata viongozi watakaokiongoza kwa miaka mitatu kwa mujibu wa katiba.

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA NASI | 0783 561 514

 
Idrisa Bandali Available On : Facebook | Instagram | Twitter
Copyright © 2013. BANDALI 44 -Haki Zote Zimehifadhiwa
Blog Hii Imetengenezwa Na Ernest James Siwigo Inamilikiwa Na Idrisa Bandali
2brothers Inc 0719766915 | 0764214303