Home » » CORTINHO AREJEA DAR AAHIDI MAKUBWA ZAIDI YANGA

CORTINHO AREJEA DAR AAHIDI MAKUBWA ZAIDI YANGA

Kiungo Andrey Coutinho, amerejea nchini jana tayari kuanza kazi na kikosi chake cha Yanga.

Mwenzake, Geilson Santana 'Jaja' ameamua kubaki kwao Brazil na nafasi yake imechukuliwa na kiungo Emerson Roque aliyetua jana pia.
Coutinho amesema anaamini ameajiandaa vizuri na ataongeza mazoezi zaidi akiwa na wenzake, pia ana hamu kubwa ya kuonyesha mabadiliko.

"Kweli nimefanya sana mazoezi, lakini bado nahitaji kuungana na wenzangu na kuendelea kujifua zaidi," alisema Coutinho akionyesha kufurahia kurejea nchini.

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA NASI | 0783 561 514

 
Idrisa Bandali Available On : Facebook | Instagram | Twitter
Copyright © 2013. BANDALI 44 -Haki Zote Zimehifadhiwa
Blog Hii Imetengenezwa Na Ernest James Siwigo Inamilikiwa Na Idrisa Bandali
2brothers Inc 0719766915 | 0764214303